Friday 29 June 2012

Tigo kuonesha burudani jijini Dar





 
TIGO KUWASHA MOTO WA BURUDANI JIJINI DAR

Na Nasser Kigwangallah, Dar es Salaam.
TIGO itawasha moto wikiendi hii katika viwanja vya Coco Beach, jijini Dar es  Salaam, ikisindikizwa na wasanii bora kabisa nchini, watakaotoa burudani safi katika fukwe ya bahari ya Hindi.
Hayo yalisemwa na Afisa Uhusiano Bi Alice Maro wakati akizungumza na waandidhi wa habari kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Alisema maadhimisho hayo ya siku mbili, ambayo ni ya mwanzo wa maonesho ya  biashara yaitwayo ‘Sabasaba’ yatafanyika kuanzia kesho Jumamosi Juni 30 na kesho kutwa Jumapili Julai 1, yataanza saa tano kamili asubuhi hadi saa kumi na mbili  jioni.
Aliwataka wasanii kutumia uwezo wao na vipaji vyao katika kuimba na kucheza sarakasi katika mashindano ya Tigo ya kusaka vipaji vya chipukizi yaliyoandaliwa kwa wote watakaohudhuria.
Au unaweza kukaa na kuburudika pamoja na wanamuziki Mr Nice na H. Baba wakati wakitumubuiza jukwaaani.
“Mwaka huu tumeamua kuwaletea burudani nyingi na za kutosha ili kuweza kuwafariji wateja wetu popote pale walipo, hivyo kufika kwao itakuwa faraja kubwa kwetu sisi,” alisema Alice Maro, Afisa Uhusiano wa Tigo.
Aliongeza kusema kuwa wanachotaka ni kwa wateja wao siyo kupata burudani tu, bali pia waje wapate na kufurahia huduma zao zilizo bora kabisa na nafuu zilizoandaliwa kwa ajili yao.
Alisema kilele cha madhimisho hayo kitakuwa siku ya Jumapili kwa burudani kutoka kwa Juma Nature, Roma Mkatoliki, Izzo B, Professor Jay, Mwasiti, Barnabas, Fid Q, Joe Makini na burudani maalumukutoka kundi la wachekeshaji la “Ze Comedy.”
Hakutakuwa na sababu ya kuondoka uwanjani jua likizama, kwani fainali za Euro mwaka 2012 zitakuwa zikianza wakati huo. Fainali hizo zitaoneshwa laivu katika skrini kubwa kuanzia saa mbili usiku.
Kiingilio ni bure kabisa na Tigo inawahamasisha wote kufika katika ufukwe wa Coco Beach ili kusherehekea na kuukaribisha msimu huu wa Saba Saba.
KUHUSU TIGO
Tigo ni mtandao wa kwanza wa simu za mkononi nchini Tanzania, ulioanza biashara mwaka 1994 na ni mtandao wenye ubunifu wa hali ya juu na bei nafuu kuliko mitandao mingine yote nchini unaotoa huduma katika mikoa 26, Tanzania bara na Visiwani.
Tigo ni sehemu ya Millicom International Cellular S.A (MIC) na inatoa huduma zake za intaneti kwa gharama nafuu kabisa na ni mtandao wenye nguvu na kasi kubwa.
Mtandao wa intaneti unapatikana maeneo mengi kwa urahisi zaidi kwa wateja wake wapaptao milioni 43 katika masoko 13 yanayoibukia barani Afrika na Amerika ya Kusini.

No comments:

Post a Comment